• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Ethiopia:Ethiopia kufanya mkutano wa kwanza na Marekani

    (GMT+08:00) 2018-07-26 19:42:00
    Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amewasili Marekani hii leo , ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kuingia uongozini.

    Abiy atakwenda Washington DC na Los Angeles katika ziara ya siku 6 itakayolenga kuimarisha uhusiano baina nchi hizo 2 .

    Kiongozi huyu aliyeingia mamlakani mwaka huu Aprili aidha ameahidi kuendelea kujenga uhusiano bora na nchi za Afrika ili kuimarisha uchumi na maendeleo ya jamii ya Ethiopia.

    Hivi majuzi Abiy Ahmed amekutana na viongozi wa Eritrea ili kuregesha uhusiano wa kidiplomasia .

    Wiki jana rais a Eritrea Isaias Afwerki alifanya ziara ya kihistoria nchini Ethiopia na mataifa hayo mawili yaliandika historia kwa kuanzisha uhusiano mpya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako