Shirika la kukabiliana na majanga la Indonesia Widyamotko limetoa taarifa kuwa watu 10 wamefariki na wengine 40 wakijeruhiwa jumapili hii katika jimbo la Magharibi la Nusa Tenggara kutokana na tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.4 katika kipimo cha Richta.
Taarifa hiyo pia inaeleza kuwa, 9 kati ya 10 waliofariki ni raia wa Indonesia na mmoja kutoka Malaysia, na kwamba vifo hivyo vimesababishwa na maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na tetemeko hilo, na kuna hofu kuwa huenda idadi ya waathirika ikaongoezeka kwa kuwa mpaka sasa vikosi vya uokozi vinaendelea na kazi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |