Naibu wa wizara ya Ulinzi ya Laos Bw. Khamliang Quthakaisone amesema kituo cha kuzalisha umeme wa maji cha Xepien-Xenamnoy kilichoko kusini mwa Laos kimeharibiwa, na kwamba mafuriko yamevikumba vijiji vingi mkoani Attapeu, na kusababisha hasara kubwa. Tume ya uokoaji iliyoanzishwa na Wizara ya Ulinzi ya Taifa imewahamisha waathirika 7,324, pia imepata miili 8 ya watu waliofariki na inawatafuta watu 123 ambao hawajulikani walipo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |