Polisi nchini Uganda wamesema watu 11 wamefariki dunia papo hapo na wengine 22 wamejeruhiwa baada ya lori walilokuwa wanasafiria kupinduka kwenye eneo la Kisoro, kusini magharibi mwa Uganda mapema jana.
Naibu msemaji wa polisi Bw. Patrick Onyango amesema lori lililokuwa limebeba wafanyabiashara 30 na bidhaa zao, lilipinduka mara kadhaa baada ya kushindwa kukata kona kali kwenye barabara kati ya Kisoro na Rubanda, karibu na kijiji cha Kigowa.
Kamanda wa polisi eneo la Kisoro Bw. Charles Okoto amesema dereva alitoroka baada ya kutokea kwa ajali hiyo, na kwamba inawezekana kuwa alikuwa anaendesha gari baada ya kunywa pombe.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |