Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang amesisitiza kuimarisha mfumo kamili wa usimamizi wa chanjo kwenye ngazi zote kote nchini.
Bw. Li amesema hayo baada ya kusikiliza ripoti kutoka kwa timu ya uchunguzi ya baraza la mawaziri kuhusu chanjo bandia ya kichaa cha mbwa inayotumika kwa binadamu, iliyotengenezwa na kampuni ya kutengeneza chanjo ya Changsheng ya mji wa Changchun.
Ripoti pia imeonesha vitendo vingi vya kampuni hiyo vya kukiuka sheria kama vile kubadilisha ovyo mchakato wa utengenezaji, kuweka rekodi ovyo za utengenezaji na ukaguzi, na kuvuruga ushahidi.
Hivi sasa, polisi wameomba ruhusa ya kuwakamata watuhumiwa wa kesi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |