Balozi wa Sweden katika Umoja wa mataifa Bw. Olof Skoog amesema Baraza la usalama la umoja huo halijafanya vya kutosha kutatua mgogoro kati ya Israel na Palestina. Bw. Skoog amesema hayo kabla ya nchi yake kumaliza muda wa uenyekiti wa zamu wa Baraza la usalama la umoja wa mataifa. Amesema kila mtu anasubiri kutolewa kwa mpango wa amani usiojulikana, na hali ya sasa inaendelea kufuata mwelekeo hasi.
Balozi huyo pia ameonya kuwa ukanda wa Gaza uko kwenye hatari kubwa ya kutokea vita, wakati mgogoro kati ya nchi hizo mbili unapamba moto kila siku.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |