Katibu mkuu wa shirikisho la soka Tanzania (TFF) Wilfred Kidau amesema anaamini kocha huyo atapendwa na watanzania wengi na amekwishaanza kufuatilia wachezaji kwa kushirikiana na benchi la ufundi.
Baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Lesotho Juni 10, mwaka jana Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam, Taifa Stars itasafiri kuwafuata Uganda kwa mechi ya Septemba 8, mwaka huu kabla ya kuwafuata Cape Verde Oktoba 10 kukamilisha mechi zake za mzunguko wa kwanza kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |