Tume ya Umoja wa mataifa nchini Iraq UNAMI imesema raia 71 wameuawa na wengine 82 wamejeruhiwa kutokana na mashambulizi ya kigaidi na mapigano ya kisilaha yaliyotokea nchini Iraq katika mwezi uliopita.
Tume hiyo imesema takwimu hizo hazihusishi idadi ya vifo na majeruhi ya askari na wanausalama wa Iraq, kwa kuwa jeshi la Iraq linakataa kutoa takwimu hizo. Hali ya usalama nchini Iraq imeboreka kidhahiri baada ya vikosi vya usalama vya Iraq kuwashinda kikamilifu wapiganaji wa kundi la Islamic State kote nchini humo mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |