Mjumbe maalumu wa Umoja wa mataifa nchini Yemen Bw. Martin Griffiths amesema atazialika pande hasimu nchini humo kushiriki kwenye mazungumzo ya kisiasa yatakayofanyika mwezi ujao mjini Geneva.
Bw. Griffiths amesema majadiliano hayo yatatoa fursa kwa pande hizo kujadili ajenda ya mazungumzo rasmi, kufikia mwafaka kuhusu hatua za kujenga uaminifu, na mipango maalumu ya kuhimiza mchakato wa kisiasa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |