Televisheni ya taifa ya Syria imesema vikosi vya ulinzi wa anga vya Syria vimetungua shabaha moja isiyotambulika magharibi mwa mji mkuu Damascus jana usiku, lakini haikutoa maelezo zaidi kuhusu shabaha hiyo.
Tukio hilo limekuja baada ya jeshi la Syria kutwaa udhibiti kamili wa mkoa wa Quneitra ulioko kusini mwa Syria karibu na milima ya Golan inayokaliwa na Israel, baada ya waasi wa huko kukubali kuondoka maeneo hayo kwenda maeneo yanayodhibitiwa nao kaskazini mwa Syria chini ya makubaliano yanayoungwa mkono na Russia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |