Watu wanne akiwemo mshambuliaji mwenywe wameuawa na wengine saba wamejeruhiwa katika mlipuko wa kujitoa mhanga uliotokea jana jioni huko Mogadishu, mji mkuu wa Somalia.
Ofisa wa polisi asiyetaka kutaja jina lake amesema mshambuliaji huyo wa kujitoa mhanga alitupa mabomu kutoka kwenye gari lililokuwa karibu na mgahawa wa Bar Itaia katika barabara ya Makkah Al Mukaramah.
Mashuhuda wamesema, gari hilo liliegeshwa mbele ya mgahawa huo unaotembelewa na wageni mara kwa mara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |