Watu zaidi ya 82 wamefariki dunia na mamia wamejeruhiwa katika tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 7.2 kwenye vipimo vya Richter lililoharibu maelfu ya nyumba na majengo katika kisiwa cha Lombok, katikati ya Indonesia.
Msemaji wa shirika la taifa la kusimamia majanga Bw. Sutopo Nugroho amesema maelfu ya watu wamekimbia makazi yao, kazi ya kuwaondoa watu walioathirika na tetememo inaendelea na majeruhi wanatibiwa nje ya hospitali ama zahanati kutokana na majengo hayo kuharibiwa au kuwa katika hali hatari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |