Klabu ya Manchester City ambao ndiyo mabingwa watetezi wa ligi kuu nchini Uingereza msimu uliopita jana imefanikiwa kushinda mechi ya ngao ya hisani ilipocheza dhidi ya Chelsea ambao ni mabingwa wa kombe la chama cha soka cha Uingereza kwenye uwanja wa Wembley mjini London.
Katika mechi hiyo ambayo inaashiria kufunguliwa rasmi kwa pazia la msimu mpya wa ligi kuu nchini Uingereza, magoli yote ya City yalifungwa na Sergio Aguero.
Mechi za ligi kuu nchini Uingereza zinatarajiwa kuanza kuchezwa rasmi jumamosi ijayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |