Timu ya Kenya iliyokwenda kushiriki mashindano ya Riadha ya Afrika nchini Nigeria imewasili jana jijini Nairobi ambapo ilipokelewa na viongozi waandamizi wa kiserikali na viongozi waandamizi wa michezo wakiongozwa na katibu mkuu wa wizara ya michezo Kirimi Kaberia.
Katika mapokezi hayo, viongozi hao waliwapongeza kwa mafanikio makubwa waliyopata mwaka huu na kuahidi kuwa wataboresha hali na hadhi ya mchezo wa riadha, pia kuboresha matukio yote yanayohusu riadha.
Kenya ilishinda nafasi ya kwanza kwenye mashindano ya riadha yaliyomalizika nchini Nigeria jumapili iliyopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |