Tume ya Uchaguzi ya Taifa ya Rwanda imetangaza majina ya wagombea 521 kabla ya uchaguzi wa wabunge utakaofanyika mwezi ujao.
Mwenyekiti wa Tume hiyo Bw. Kalisa Mbanda amesema orodha hiyo inajumuisha watu 302 kutoka vyama mbalimbali vya kisiasa, wagombea huru 4, 26 kutoka kundi la vijana, 10 kutoka kundi la walemavu na wagombea wanawake 179. Chama tawala cha RPF kimewateua wagombea 70 na vyama washirika wake vina wagombea 10.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |