Wapiganaji wawili wa kundi la Hamas la Palestina jana waliuawa katika shambulizi la mizinga lililofanywa na jeshi la Israel kaskazini mwa Ukanda wa Gaza.
Brigedi ya al-Qassam iliwatambua wapiganaji hao wawili waitwao Ahmed Murjan na Abdul Hafiz al-Selawy kutoka kambi ya wakimbizi ya Jabaliya, kaskazini mwa Gaza.
Israel haijatoa maoni kuhusu shambulizi hilo. Lakini vyombo vya habari nchini humo vimesema kuwa jeshi la Israel lilishambuliwa karibu na eneo la mpaka kaskazini mwa Gaza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |