Kitengo cha vikosi maalumu vya Somalia Danab kinachoungwa mkono na vikosi vya Umoja wa Afrika kimefanya shambulizi dhidi ya maeneo ya al-Shabab magharibi mwa mji wa Balad katika eneo la Middle Shabelle, kusini mwa nchi hiyo. Kamishna wa mji wa Balad Bw. Nuur Shueb amesema katika operesheni hiyo, vikosi washirika vimedhibiti vijiji vinne ambako wapiganaji wa al-Shabab wamekuwa wakifanya mashambulizi mbalimbali kwa miezi kadhaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |