Waziri wa mambo ya nje wa nchi wanachama wa Shirika la Maendeleo la Kiserikali la Nchi za Afrika Mashariki IGAD leo mjini Khartoum watashiriki katika mkutano wa dharura kwa ajili ya kuandaa kuanzisha raundi mpya ya mazungumzo kati ya makundi hasimu nchini Sudan Kusini. Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Bw. Mohamed Abdalla Idris amesema mkutano huo utajadili mpango wa kutekeleza makubaliano ya amani ya Sudan Kusini, yaliyofikiwa mjini Khartoum na kupanga vipaumbele kuhusu masuala muhimu ambayo hayajatatuliwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |