Mchezaji namba moja kwa viwango vya ubora wa tennis nchini Uingereza Andy Murray ameondolewa kwenye raundi ya kwanza ya mashindano ya Cincinnati Masters yanayoendelea nchini Marekani baada ya kufungwa na Lucas Pouille wa Ufaransa.
Lucas alishinda kwa seti ya alama 6-1 1-6 na 6-4, na katika mechi nyingine zilizofanyika jana Kei Nishikori wa Japan alimshinda Andrey Rublov wa Urusi, na Pablo Carreno Busta wa Hispania alimshinda Richard Gasquet wa Ufaransa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |