Kuelekea michezo ya jumuiya ya Afrika Mashariki inayotarajiwa kuanza kesho nchini Burundi, Wizara ya habari, utamaduni, sanaa na michezo ya Tanzania imetoa orodha ya majina ya wachezaji wa timu za Tanzania wanaokwenda kushindana.
Timu hiyo itaongozwa na maafisa wa serikali wanne, huku kiongozi wa msafara ni Khamis Ali Mzee kutoka Baraza la Michezo la Tanzania (BTMZ)
Katika wachezaji hao, 10 watawakilisha upande wa riadha, 23 wanawake na wanaume mpira wa miguu, upande wa karate ni wachezaji 7, na netiboli wachezaji 14.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |