Adesina alisema ubadilishanaji wa teknolojia unahitajika na kwamba ushahidi kutoka nchi kama vile Nigeria umeonyesha kuwa teknolojia pamoja na kujitolea kwa serikali tayari kumeanza kuzaa matunda.
Adesina aliyasema haya jana wakati akizungumza katika Mkutano wa mwaka wa Chama cha Kilimo na Sayansi ulioandaliwa jijini Washington D.C.
Adesiana alisema Nigeria,ambako sera wakati wa utawala wake kama Waziri wa Kilimo,zilichangia katika mabadiliko ya uzalishaji wa mchele katika kipindi cha miaka mitatu.
Adesina alisisitiza kuhusu azma ya Benki ya AfDB ya kubadilisha sura ya kilimo barani Afrika ili kufungua vyanzo vyenginevyo vya utajiri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |