• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Serikali inashughulikia miundombinu Kilombero

    (GMT+08:00) 2018-08-16 20:13:40
    Miundombinu mibovu ambayo inaathiri uzalishaji wa sukari na usafirishaji wake hadi sokoni hivi karibuni itaboreshwa wakati serikali ikiwa mbioni kutekeleza azma yake ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda na yenye uchumi wa kipato cha kati kufikia mwaka 2025.

    Naibu Waziri wa Kilimo,utoshelevu wa chakula na vyama vya ushirika,Omar Mgumba amesema wizara yake inaelewa kuwa wakulima wa miwa wameshindwa kuuza bidhaa hiyo kwa kiwanda cha sukari cha Kilombero kwa sababu barabara na madaraja hayapitiki.

    Alisema uboreshwaji wa miundombinu pia utasaidia kiwanda hicho kusafirisha sukari sokoni kwa urahisi haswa maeneo ya mijini.

    Alisema serikali inajitahidi kuhakikisha kuwa inaboresha miundombinu katika wilaya ya Kilombero na mkoa wa Morogoro ili wakulima waweze kuuza miwa katika kiwanda cha Kilombero wakati wowote.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako