WQakfu wa Tony Emelu umetangaza tarehe 25 Oktoba kuwa tarehe ya mkutano huo wa ujasiriamali,unaotarajiwa kuvutia maelfu ya wajasiriamali wanaochipuka kutoka sehemu mbalimbali za Afrika,wengi wao wakiwa ni walionufaika na wakfu huo.
Wakfu wa Tony Emelu,ambao unatoa msaada wa ujasiriamali wa $100 milioni unalenga kuwawezesha wajasiriamali 10,000 waafrika katika kipindi cha miaka 10.
Kila mwaka wakfu huo huchagua wajasiriamali 1,000 kutoka sehemu mbalimbali za Afrika kupata mafunzo ya wiki 12,ushauri,na kuwapa mtaji wa $10,000 .
Mkutano huo wa TEF huwa ndio mwisho wa ratiba ya kila mwaka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |