Ndovu ya Ivory Coast na Amavubi wanatarajiwa kushuka dimbani Septemba 7 uwanja wa Amahoro nchini Rwanda katika mechi ya kusaka tiketi ya kucheza michuano ya kombe la Afrika mwakani yatakayofanyika nchini Cameroon.
Niyonzima amesema, ni vigumu kwasababu umepita muda mrefu bila Amavubi kucheza mechi yeyote ya kujipima nguvu. Ameaomba viongozi wa shirikisho la mpira wa miguu Rwanda (FERWAFA) kuandaa mechi za kirafiki kwani zinawasaidia wachezaji kuelewana, na kocha kujua timu yake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |