Wizara ya ulinzi ya Russia imesema kituo cha kijeshi cha Hmeimim cha Russia nchini Syria kimeangusha ndege 45 zisizo na rubani UAV katika mwezi uliopita.
Msemaji wa wizara hiyo Meja Jenerali Igor Konashenkov amesema, mwezi uliopita ndege 45 zilizobeba mabomu ziliangushwa kwa njia ya mfumo wa mionzi, tano kati yao zilitunguliwa katika siku tatu zilizopita.
Msemaji huyu amesema majaribio ya mashambulizi ya kigaidi yanayotumia ndege zisizo na rubani yameongezeka katika mwezi uliopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |