Bondia wa ngumi za kulipwa nchini Tanzania, Mada Maugo amemchapa kwa pointi mpinzani wake Charles Misanjo wa Malawi katika pambano la kimataifa la uzito wa Super Middle weight kwenye ukumbi wa PTA jijini Dar es salaam.
Akizungumza baada ya pambano hilo, Misanjo amekataa kushindwa na kulalamikia ushindi wa Maugo akisema amependelewa na majaji wa pambano hilo. Amesema Tanzania wakiendelea hivi ni wazi kuwa wanaua mchezo wa ngumi nchini humo kutokana na maamuzi mabovu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |