• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania:Huawei kutoa mafunzo ya ICT kwa wakufunzi wa vyuo vikuu

    (GMT+08:00) 2018-08-22 20:17:54

    Vyuo vikuu kadhaa nchini Tanzania vinatarajia kuanza kutoa mafunzo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT),ili kukuza vipaji vya vijana.

    Mpango huo ambao unashirikisha kampuni ya Huawei unalenga kutatua changamoto mbalimbali kupitia wataalamu wake duniani ikiwa ni pamoja na kutumia nyenzo za kitaalamu.

    Mradi huo unaofahamika kama "Seeds for the Future" ulianzishwa miaka mitatu iliyopita ambapo jana ulizinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam.

    Akizungumza wakati wa uzinduzi huo,Mkurugenzi Mtendaji wa Huawei,Gao Mengdong alisema kampuni yake ina wajibu wa kutoa huduma kimataifa.

    Alisema Huawei itatoa mafunzo ya wakufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM),Taasisi ya Ufundi Dar es Salaam (DIT),na Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA),ili kuwapa ujuzi katika kozi mbalimbali za ICT.

    Aidha Mengdong alisema anaamini kuwa hii italeta mabadiliko chanya katika maendeleo na ukuaji wa uchumi nchini Tanzania.

    Alisema kila mwaka mpango huo hutoa fursa kwa wanafunzi 10 wa vyuo vikuu kutoka Tanzania kwenda Beijing,China kutembelea shughuli mbalimbali za Huawei katika makao makuu yake mjini Shenzhen.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako