• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wanyarwanda zaidi ya 100,000 kunufaika na mradi wa kilimo wa AfDB

    (GMT+08:00) 2018-08-23 18:30:30
    Wakulima wadogo,wasindikaji wa bidhaa za kilimo,mahoteli,na migahawa hivi karibuni huenda hivi karibuni huenda vikaongezeka kufuatia kuzinduliwa kwa maradi wa mabilioni ya fedha unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).

    Mradi huu unalenga kuongeza teknolojia kwa ajili ya mageuzi ya kilimo Afrika katika mnyororo wa thamani wa maharage,machungwa na viazi vitamu.

    Mradi huu,katika nchi 12 barani Afrika,unalenga kusaidia mkakati wa benki ya AfDB wa kulisha Afrika ili bara hilo liweze kupunguza uagizaji mkubwa wa chakula. Hii itafanikishwa kupitia upigaji jeki wa uwezo wa kilimo Afrika.

    Mtafiti Mkuu katika Bodi ya Kilimo ya Rwanda ,Augustin Musoni, alisema kuwa mpango huo utawanufaisha watu zaidi ya 100,000 watakaowekwa katika makundi ya kaya 30,000 nchini Rwanda.

    Alisema watakaonufaika ni wale walio katika mnyororo wa thamani wa baadhi ya mimea kwa kupatiwa teknolojia muafaka za uzalishaji chakula.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako