• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Wadau wa uchukuzi wa anga kukutana Nairobi

    (GMT+08:00) 2018-09-04 19:39:14

    Wadau wa sekta ya uchukuzi wa ndege barani Afrika wanatarajiwa kukutana nchini Kenya wiki ijayo kujadili usimamizi wa sekta hiyo huku Umoja wa Afrika ukiendelea kusuuma ajenda ya kuwa na anga huru barani humo.

    Mkutano huo utakaoandaliwa na Shirika la Huduma za Usafiri wa anga na utaleta pamoja wakuu wa mashirika uya ndege kutoka zaidi ya nchi 30 za Afrika.

    Mkuu wa mamlaka ya usafiri wa anga nchini Kenya Gilbert Kibe amesema watajadili lengo la Afrika la kufikia mfumo wa usafiri salama wa anga, utaalum, na ushindani wa gharama nafuu.

    Mkutano huo utafanyika chini ya wenyekiti wa Hamza Johari, ambaye ni mkurungezi wa mamlaka ya usafiri wa anga nchini Tanzania.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako