Timu ya taifa ya Wales imeifunga bila huruma timu ya taifa ya Ireland magoli 4-1, Gareth Bale amefunga moja kati ya magoli hayo manne na kufikisha jumla ya magoli 30 katika timu hiyo.
Uholanzi nayo imeichezesha mchakamchaka Peru na kuibuka na ushindi wa magoli 2-1.
Ureno wakicheza bila Christiano Ronaldo, wamelazimika kumtumia Pepe kusawazisha goli dakika ya 32 baada ya Ivan Perisic kutangulia kuwafungia Croatia katika dakika ya 18. Hadi mwisho wa mchezo, Ureno imetoka sare za Croatia ya goli 1-1.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |