• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Soka, Ligi ya mataifa ya Ulaya: Ureno bila Ronaldo yashinda 1-0 dhidi ya Italia

    (GMT+08:00) 2018-09-11 09:12:36
    Timu ya taifa ya Ureno bila ya Ronaldo jana imefanikiwa kupata ushindi goli 1-0 dhidi ya Italia kwenye mechi ya hatua ya makundi ya ligi ya mataifa iliyofanyika katika uwanja wa Luz mjini Benfica.

    Goli la Ureno lilifungwa na Andre Silver kunako dakika ya 48 ya mchezo huo, na katika mechi nyingine zilizochezwa jana Sweden ikiwa nyumbani jana imefungwa magoli 3-2 na Uturuki.

    Scotland nayo imeanza vyema mashindano hayo kwa kupata ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Albania, Monteenegro ikishinda 2-0 ilipocheza na Lithuania, Serbia na Romania zikitoka sare ya 2-2, na sare nyingine zikiwa ni 1-1 kati ya Andorra na Kazakhistan, 1-1 Malta na Azerbaijan.

    Lakini mambo yalikuwa mazuri kwa timu ya Kosovo ambapo mchezaji wao wa kutegemewa Atdhe Nahiu anayecheza klabu ya Sheffield Wednesday ya Uingereza alifunga magoli yote mawili ya ushindi wa 2-0 timu hiyo ilipokuwa nyumbani kucheza na timu ya taifa ya visiwa vya Feroe.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako