Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta jana ametuma salamu za pole kwa wanamichezo nchini Kenya, na kueleza masikitiko yake kutokana na kifo cha kiongozi wa michezo ambaye zamani alikuwa bingwa riadha nchini Kenya Major Paul Koech.
Katika barua yake ya salama, Kenyatta ameandika kuwa Koech alikuwa mtu anaeipenda kazi yake na ametoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya riadha na michezo kwa ujumla nchini Kenya.
Mpaka umauti unamkuta wiki iliyopita kutokana na maradhi ya ubongo, Paul Koech alikuwa na miaka 49, na alikuwa makamu wa Rais wa chama cha michezo cha Majeshi ya Kenya, na amezikwa jana kwa heshima za kijeshi nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |