Wakati jana kocha mkuu Manuel Pellegrini akiadhimisha umri wa miaka 65, timu yake ya West Ham united ilipata ushindi mnono wa magoli 3-1 ambao ni wa kwanza kwa timu hiyo tangu msimu huu uanze.
West Ham ilipata ushindi huo ikiwa ugenini dhidi ya Everton.
Magoli ya West Ham ambayo imefungwa katika mechi zake nne zilizotangulia jana yalifungwa na Andry Yarmolenko aliyefunga mawili na moja likifungwa na Marko Arnautovic.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |