Mwakilishi maalumu wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan Bw. Tadamichi Yamamoto, amesema changamoto za kisiasa zinaweza kuvuruga uchaguzi wa wabunge utakaofanyika mwezi ujao nchini humo, kama viongozi wote wa kisiasa hawatafanya juhudi za kiujenzi na kiamani kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa wakati. Tume ya Uchaguzi imetangaza kuwa watu zaidi ya milioni 9 wameandikishwa kupiga kura.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |