Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesitisha UCHAGUZI wa viongozi wa klabu ya Simba uliopangwa kufanyika Novemba 3, mwaka huu kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kukiukwa kwa baadhi ya taratibu za msingi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa TFF, Revocatus Kuuli amesema kwamba miongoni mwa mapungufu hayo ni ada ya uanachama kwa ngazi ya Uenyekiti pamoja na Wajumbe kutofautiana, jambo ambalo ni kinyume na matakwa ya klabu pamoja na TFF.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |