Inaelezwa kuwa, kwa uzoefu wa kanuni na sheria zinazoongoza nchini Italia, mchezaji wa Juventus Douglas Costa huenda akafungiwa kutocheza mechi tano za mashindano ya FA ya Italia, pamoja na faini ya fedha Yuro 200,000 kutokana na kitendo ambacho si cha kiuanamichezo.
Costa alitenda makosa matatu tofauti, kwanza alimpiga kwa kiwiko cha mkono, amkatolea maneno ya dhihaka na kisha kumtemea mate mchezaji mwenzake.
Licha ya kupewa kadi nyekundu kwenye mechi hiyo, licha ya kuiomba radhi jamii na licha ya klabu kumtetea kuwa alikasirishwa na maneno ya dhihaka dhidi yake, Douglas huenda akaadhibiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |