• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wafungwa

    (GMT+08:00) 2018-09-18 19:08:49

    Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umefungwa leo huko New York, ambapo Bibi Maria Fernanda Espinosa kutoka Ecuador ameapishwa kuwa rais wa awamu ya 73 ya baraza hilo.

    Kwenye mkutano na waandishi wa habari, bibi Maria amesema kuwa, atafanya kazi kwa bidii kulinda maslahi ya pande nyingi na kuufanya umoja huo kuwa na manufaa kwa watu wote.

    Rais wa baraza hilo anayemaliza muda wake Bw. Miroslav Lajcak katika hotuba amesema, Umoja wa Mataifa umejengwa kwa msingi wa mazungumzo, nchi wanachama wake wanapaswa kujadili migongano kwa njia ya mazungumzo badala ya vita.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako