• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya-Makampuni ya simu yapewa siku 2 kuzima wateja ambao hawajaandikishwa

    (GMT+08:00) 2018-09-19 18:53:59

    Kampuni zinazotoa huduam za simu nchini Kenya zimepewa hadi ijumaa kuwaondoa wateja ambao hawajasajiliwa na wale wanaotumia stakabadhi bandia,au wakabiliwe na faini ya asilimia 0.02 ya mauzo yao ya mwaka.

    Mamlaka ya Mawasiliano nchini Kenya imesema ukaguzi katika mitandao ya simu ya Safaricom,Airtel,na Telkom umebaini kuwa taarifa kuhusu wateja haziko sahihi,na pia kuna kadi za simu ambazo hazijasajiliwa,na hivyo kusaidia katika vitendo vya uhalifu.

    Makosa yaliyopatikana ni pamoja na kadi za simu ambazo zimesajiliwa mara mbili au zaidi chini taarifa za watu tofauti,kutowiana kwa nambari za usajili kwa kutumia pasipoti na vitambulisho vya raia wa kigeni na pia waendeshaji kukosa kuwadhibiti mawakala wao.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako