Watoto na vijana milioni 300 wenye umri wa miaka mitano hadi 17 hawaendi shule, ambao theluthi moja yao wanatoka nchi zinazoathirika na migogoro au maafa na kufika milioni mia moja.
Hayo yamo kwenye ripoti iliyotolewa na Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF kwenye ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 73 wa Umoja wa Mataifa. Ripoti hiyo inafuatilia hali ya sasa ya watoto na vijana wasioenda shule kote duniani, ikisisitiza kwamba umaskini bado ni kizuizi kikuu kwa elimu ya kimataifa. Aidha imesema ni chini ya asilimia 4 ya msaada wa kibinadamu iliyotumiwa kwenye sekta ya elimu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |