Tume ya Umoja wa Mataifa nchini Libya (UNSMIL) imekaribisha mpango wa mageuzi ya kiuchumi uliopitishwa na Baraza la Rais, kwa kushauriana na Benki Kuu ya Libya, baraza la wawakilishi na baraza kuu la taifa ili kuanza utekelezaji wa mageuzi ya kiuchumi.
Tume hiyo imesema hayo kwenye taarifa na kuongeza kwamba inatarajia marekebisho hayo yataweza kuboresha maisha ya Walibya nchini kote.
Mpango huo ni pamoja na kubadilisha kiwango cha ubadilishaji wa fedha dhidi ya fedha za kigeni kwa kuagiza ada za ununuzi wa fedha za kigeni, na kushughulikia ruzuku ya serikali kwenye mafuta
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |