Waziri mkuu wa Palestina Bw. Rami Hamdallah ametoa wito kwa nchi za Umoja wa Ulaya kutambua taifa la Palestina lenye mji mkuu Jerusalem Mashariki, ili kuokoa "mpango wa mataifa mawili" wakati Israel inapanua ujenzi wa makazi ya Wayahudi na kuchukua kwa nguvu ardhi za Palestina zilizo Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Amesisitiza kuwa Marekani kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel na kusitisha kutoa msaada wa kifedha kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Msaada na Kazi kwa Wakimbizi wa Palestina UNRWA ni "adhabu ya pamoja" dhidi ya wananchi wa Palestina.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |