• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya:Wamiliki wa simu zisizoandikishwa kufungiwa huduma

    (GMT+08:00) 2018-09-20 19:49:17
    Kampuni za simu za mkononi zimepewa hadi siku ya ijumaa wiki hii kuwafungia huduma wateja wao wote ambao hawasajiliwa ama kuandikishwa kwa vyombo sahihi vya mawasiliano.

    Halmashauri ya mawasiliano ya Kenya imearifu ukaguzi mkuu uliofanywa kwa kampuni za Safaricom,Airtel na Telkom umebainisha kuna baadhi ya watumiaji wa simu hizo ambao hawasajiliwa.

    Baadhi ya hitilafu zilizopatikana ni pamoja na simu kadi kupatikana na watumiaji zaidi ya wawili,mvurugano wa tofauti kati ya wamiliki wa simu hizo wanaotoka nje ya nchi ,pamoja na tofauti kati ya waendeshaji wa simu na maajenti.

    Francis Wangusi amesema kufikia Ijumaa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya uhalifu wa aina yoyote wa simu za mkononi.

    Faini ya laki moja aidha itatolewa kwa watakaopatikana kukikuka amri hii.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako