Tume ya Umoja wa Mataifa nchini Libya UNSMIL imeonya kuhusu mashambulizi dhidi ya makazi ya watu mjini Tripoli, wakati makundi hasimu yanaendelea kupambana. Tume hiyo pia imeyakumbusha makundi hayo kuhusu makubaliano waliyofikia ya kusimamisha vita na kusema kuhatarisha usalama wa raia hakukubaliki kwenye Sheria ya Ubinadamu ya Kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |