Nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wametoa wito kwa Israel kufikiria tena uamuzi wake wa kubomoa kijiji cha Khan al-Ahmar cha Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi.
Nchi hizo zimesema kwenye taarifa ya pamoja kuwa matokeo ya kubomolewa kwa kijiji hicho na kuwafanya watu wakiwemo watoto wapoteze makazi, ni jambo kubwa na linaweza kutishia uhai wa suluhu ya mataifa mawili na kuvuruga mustakabali wa amani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |