Kocha wa timu ya taifa ya waendesha baiskeli Sempoma Felix ametangaza wachezaji watano watakaoenda nchini Cameroon katika shindano la mbio za baiskeli zinazojulikana kama Grand Prix Chantal Biya.
Shindano hilo litaanza Septemba 26 hadi 30 mwezi huu ambalo ni la kila mwaka na limepewa jina la mke wa rais wa Cameroon Paul Biya lilianzishwa mwaka 2011.
shindano hilo litakuwa na sehemu tano ambazo ni
Sehemu 1: itakuwa mjini Douala ambapo ni la kilomita 92
Sehemu 2: litaanzia mjini Yaounde-Nanga- na kumalizikia mjini Eboko, 152 km
Sehemu 3: mjini Yaounde – Ebolowa, 151 km
Sehemu 4: mjini Samgmelima – Meyomessala, 134 km
Sehemu 5: mjini Sangmelima – Yaounde, 170 km
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |