Rais Edgar Lungu wa Zambia jana amesema, China ni mwenzi mkubwa wa ushirikiano wa Zambia, na mradi wa utoaji wa maji wa Kafulafuta uliojengwa na China kwa msaada wa kifedha wa China utawanufaisha wazambia.
Rais Lungu amesema hayo wakati aliposhiriki kwenye uzinduzi wa ujenzi wa mradi wa Kafulafuta. Amesema mradi huo utatoa maji safi ya kunywa kwa wakazi wa karibu, pia utaleta nafasi nyingi za ajira na fursa nyingi za biashara. Mradi huo umeungwa mkono na serikali ya China na kampuni za China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |