Salome Nyirarukundo wa Rwanda ameandika rekodi mpya kwenye mbio za Marathon za Montreal nchini Canada baada ya kushinda na kutumia muda mfupi zaidi wa saa 2 dakika 28 na sekunde 2.
Mshindi wa pili alikuwa Joan Kigen kutoka Kenya, na Emebet Antenech kutoka Ethiopia akishika nafasi ya tatu.
Kwa upande wa wanaume Ezekiel Mutai kutoka Kenya alishika nafasi ya kwanza, Wycliff Biwott kutoka Kenya pia akishika nafasi ya pili na nafasi ya tatu ikienda kwa Jean Marie Vianney kutoka Rwanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |