Rais wa Shirikisho la Kandanda Duniani – FIFA Gianni Infantino ametoa wito kwa shirikisho lake kufanya juhudi zaidi za kuyasaidia mabara ya Amerika Kusini, Afrika na Asia kushindana dhidi ya Ulaya katika Kombe la Dunia
Infantino amesema FIFA inapaswa kuboresha kandanda, sio tu mashindano bali pia katika ngazi ya juu kote duniani na kuwekwa kipaumbele katika kusonga mbele.
Naye kocha wa Morocco Mfaransa Herve Renard amekiri kuwa kunahitajika mpango wa utekelezaji akiongeza kuwa pengo linazidi kuwa kubwa lakini haoni kama kutanua Kombe la Dunia hadi timu 48 kimsingi ni wazo zuri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |