Kampuni 45 za China zitaanza kununua mbaazi kutoka Tanzania.
Wawekezaji hao wa China wamesema wapo tayari kununua bidhaa za mazao mengine kama kahawa, asali, tangawizi, mihogo, soya na chai yakiongezewa thamani.
Taarifa hizo zimebainishwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tantrade) mwishoni mwa wiki hii.
Mkurugenzi mkuu wa Tantrade, Edwin Retageruka amesema kampuni hizo zimeeleza utayari huo kwenye maonyesho ya China-Asean Expo (CAEXPO) yaliyofanyika Septemba 12 hadi 15 mwaka huu jijini Nannang, China ambako mashirika 23 ya umma na wafanyabiashara walihudhuria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |