Rais Moon Jae-in wa Korea Kusini amesema Korea Kaskazini imeamua kuacha mpango wake wa nyuklia na nia hiyo ni imara.
Akizungumza na wanahabari kabla ya kukutana na rais Donald Trump wa Marekani jana katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, rais Moon amesema kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong Un anatarajia kukutana na rais Trump mapema iwezekanavyo ili kushirikiana na Marekani kukamilisha kazi za kuondoa silaha za nyuklia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |